Friday, March 29, 2013

KUTOKA KWA OBAMA

WASANII WATANO WENYE MKWANJA MREFU 2013 KUTOKANA NA FORBES

Sean" Diddy" Combs amekuwa wa kwanza kwa mwaka huu ametajwa kwenye list ya Forbes ya wasanii 5 wenye mkwanja, anakadiriwa kuwa na dola milioni 580. Akiwa yeye ndo mwanzilishi wa Bad Boy, mkwanja wake mwingi unatokana na kinywaji chake cha Ciroc.
Namba 2 imeenda kwa Shawn Jay-z” Carter anamiliki dola milioni 475 na anaendelea kushikilia hisa kwenye kampuni ya Roc Nation, Carol’s Daughter, Brooklyn Nets na vitu vingine kikubwa zaidi ni Barclays Center yenyewe, pia ameongeza ushirikiano na Duracell, Budweiser na Barcadi D’usse Cognac.

Namba 3 imeenda kwa Andre “Dr Dre” Young anamiliki dola milioni 350, anashukuru sana headphones zake za Beats By Dre. Mwaka mmoja baada ya kuuza asilimia 51 ya kampuni kwa watengenezaji wa simu HTC kwa dola milioni 300 uwezekaji wao unaendelea kukua kwa faida kutokana na kufanya vizuri zaidi kwa asilimia 65 kwa share nzuri ($99 na zaidi) katika soko la headphones.

Bryan “Birdman” Williams anashikilia namba 4 na kamapuni yake ya Cash Money Young Money inakuwa anamiliki dola milioni 150. YMCMB anapatikana Drake, Nicki Minaj na Lil Wayne. Birdman pia kw sasa amezindua YMCMB clothing line inafahamika na kinywaji kikali kinachofahamika kama GT Vodka.

Akifunga list katika wasanii watano wenye mkwanjwa walitajwa na Forbes anashikilia Namba 5 “Curtis “50 Cent” Jackson” anmiliki dola milioni 125. Mkwanja wake huo unatokana na kuuza sana muziki wake, Biashara, video games na vitabu vilivyotokana na album yake ya Get Rich Or Die Tryn” na uwekezaji aliolipwa na Vitamin Water parent Glaceau kwa Coca cola mwaka 2007.

No comments:

Post a Comment