Friday, October 27, 2017

MPANDA NGAZI HUSHUKA

NAKALA HII BADO IPO KWENYE MABORESHO.
                                               
Ngazi ni kifaa ambacho hutumika kuzifikia sehemu za juu ambazo hazifikiki kiurahisi. Sehemu za juu aidha huwa na kitu muhimu sana kwa wakati huo au Mda wote. 

Binadamu wa kileo hutumia sana Ngazi, Lakini si ngazi hizo tunazo zifahamu kufikia mafanikio ambapo dhuluma,  ukandamizaji, unyang'anyi,  udanganyifu na mengine mengi sana mabaya ambayo Binadamu huyafanya Ili kujiingizia kipato kiurahisi pasipo kufanya jitihada zozote. 

Inasikitisha sana kuona mataperi wanazidi kuongezeka siku hadi siku,  watu wanakaa wanajadili namna ya kuingiza kipato pasipo kuvuja jasho. 
Magufuli amefanya juhudi kubwa ya kutengeneza Tanzania mpya lakini bado wasio na taaluma au uelewa wanaliwa pesa pasipo kujua wanaliwa.

Usipo kuwa makini ukajikuta unatoa fedha pasipo kuwa na haja ya kutoa pesa.  Matapeli wanakaa wanajadili namna ya kuingiza kipato pasipo kufanya jitihada zozote. je ?  unapenda kutapeliwa. Kama jibu ni Hapana Bhaaasi endelea kufuatilia nakala hii 

Saturday, July 23, 2016

You gonna have some ups and some downs...


DRAFT 1.
You have to trust on something, this basically rely on spiritual believes on GOD. One of the secrets to do a great thing is you must find what you love, if you didn’t find yet  keep looking  and don’t stop until you find it, have a courage to follow your heart and your intuition.


In life you gonna have some Ups and some Downs, most people give up on themselves easily, you know that human spirit is powerful, it hard to kill human spirit, anybody can feel good when they have their good health condition, who has happy relationship with husband or wife (good family relationship), anybody can be positive there, anybody can have large vision there, any body can have the ability to provide solution to several matters although the correctness will rely on his/her knowledge and sometime they can   influence others on the wrong direction due to overconfidence and faith.  
   

The real challenge of growth mentally, emotionally, spiritually comes when you have knocked down it need courage to start over again. it take time to start over again, fear kills dreams, fear kills hope, fear put people in hospital, fear can  hold you back from doing something that you know that you are capable of doing but will colorize you.  At the end of feeling is nothing but at the end of every principle is  promise, behind of every principle is the promise .

Discipline your emotion because if you don’t discipline your emotion they wanna use you, it is not easy but if you are serious enough you wanna win.  Say NO to your dream you might push back your dream, don't allow your emotional to contol you, we are all emotional but we wanna begun to discipline emotional, if you don't win, this is what we should stand for, live your life with passion, it doesn't matter of what happens yesterday or what happens now, what matter is what you wanna do about it JUST STAND FOR YOUR DREAM. Accept where you are and live your life with passion.

From Millionaire Mindset  of view.



Awadhi Chang’a.

2016

Saturday, May 2, 2015

TENDEA HAKI TAALUMA YAKO.


SAIDIA JAMII, JAMII ITAKUSAIDIA.

Mchakato wa kuleta mabadiliko katika jamii husaidia wataalamu kuzifikia ndoto zao za maisha bora kwa sababu jamii hiyo unayoisaidia automatically will pay you back kwa maana jamii inahitaji msaada mkubwa kutoka kwa wataalam mbalimbali, kwa sababu kuna matatizo mbalimbali yanayotuzunguka ambayo hayajapatiwa suruhisho hadi sasa. je huamini kama jamii itakupa manufaa kwa kuisaidia anza sasa na utaona mabadiliko makubwa sana katika maisha yako.

Huu ni mchakato maalum kwa ajili ya kuwaelimisha wataalama ili waweze kusaidia jamii zao zinazowazunguka, kwa maana hadi sasa mambo mengi ya kusaidia jamii na mazingira yanayowazunguka  yanafanywa na mashirika ya kigeni ya wazungu, wachina n.k... kwa mfano WCS, WWF ni mashirika ambayo makao makuu yako nchi za nje, Hii inadhihirisha dhahiri kwamba tumetawaliwa hadi kifikra na mtazamo kwa sababu tumeziacha fikra zetu zilale na kusababisha wageni kuja kutufanyia mambo ya kusaidia jamii na mali asili zetu ili zisipotee, ni jambo la kusikitisha sana kuona sisi wenyewe hatuoni umuhimu wa kuwa pamoja ili kuipigania nchi yetu na kutunza mali asili zetu na kuijenga nchi yetu kwa manufaa yetu wenyewe, ivi unadhani huyo mgeni atafanya hizo kazi kwa uchungu bila kuiba rasilimali zetu. amka wewe mtaalam wa kitanzania jengeka kifikra acha kubaki na vitu vizuri katika kichwa bila kuvitoa kwa jamii ili visaidie kujenga jamii yetu ili tusiendelee kuwategemea wageni. wageni hawa hawawezi kuwa na uzalendo asilimia mia 100%.

Angalia leo dola ya Mmarekani inavonyanyasa shilingi ya kitanzania Ambapo dola moja 1 ni sawa na shilingi elfu mbili 2,000. Acha kulalamika umaskini wakati wewe mwenyewe ndo unayeikubali hali hii ya maisha kwa maana kufanya kazi kwa bidii ndo zao la maisha bora jitume kusaidia jamii, kujenga fikra zako mwenyewe na za wengine.

Wasomi au wataalam waliowengi walitegemeamambo makubwa sana siku zao za usoni hasa pale wanapo anza kupata taaluma zao na baada ya kuanza kufanya kazi zao zinazowaingizia kipato. Mtazamo huu ni mzuri sana lakini kuna changamoto nyingi sana ambazo huwakabili wataalam walio wengi na kujikuta wamekata tamaa kuzikamilisha ndoto zao za maisha bora. Hii husababishwa na wataalam kuto kujua maslai ya kuisaidia jamii, hakuna jambo lolote linalolipa hapa duniani kama kusaidia jamii na mazingira yake. Lazima tujue kusaidia jamii ndo kipaombele cha taaluma zetu tunazopewa mashuleni na walimu Kwa hiyo baasi taaluma ni msingi wa kuleta mabadiliko na kutatua changamoto za maisha ya jamii na mazingira yake. lakini wataalam au wasomi walio wengi wanakabiliwa na tatizo la kulala kwa fikra ambazo ni za muhimu sana katika taifa letu. tafadhari amsha fikra zako acha kulaza fikra zako ni hasara kubwa sana kwa taifa letu.

Wataalam wanafikra nzuri na wanafahamu mbinu za kujiimarisha kifikra lakini fikra  zao mala nyingi hulala kwa sababu ya mambo mengi ya kiteknolojia. Waliowengi wanajikuta addicted kwa baadhi ya vitu vya kisasa ambavyo kimsingi havimsaidii kumjenga kifikra na mitazamo ya kuiendeleza taaluma yake ili aisaidie jamii kwa mfano kuwa addicted na matumizi ya social media.

Jambo lingine wataalam waliowengi wanavipa vipaombele vitu ambavyo ambavyo haviimarishi taaluma zao na fikra zao. Katika mijadara yao ya kila siku hujikuta wakijadili mambo ya burudani kwa mfano Dimond Platnum anatoka na nani. Mijadala isiyo na mantiki husaidia katika kudumaza taaluma zao kwa maana mala nyingi mijadala husaidia kuamsha fikra zilizo lala kwa maana ili jambo liwe kwenye utekelezaji wa mtu binafsi linahitaji kukumbushwa mala kwa mala ili akili ipate kuliona umuhimu wa jambo hilo.Vile vile wataalam hao hao katika mijadala ya makundi mbalimbali ya jamii wao ndo wamekua mstali wa mbele kuongoza ama kusapoti mijadala isiyo na tija, hatukatai kuongelea mambo pendwa lakini yasiwe ndo msingi wa mazungumzo yenu kwa sababu yatadumaza fikra za maendeleo. Tusipokua makini tutaendelea kumtegemea mzungu katika kutuendeshea mambo yetu na sisi tutabaki tukipiga polojo tu zisizo na maana. TAFADHARI USIPIGE POLOJO TOA FIKRA JENZI.

 KUWA MZALENDO SAIDIA JAMII JAMII ITAKUSAIDIA

ITAENDELEA TOLEO LIJALO
yafuatayo yatakuwemo
1. namna ya kujijenga kifikra
2. namna ya kutumia taaluma yako kuisaidia jamii
3. ni kwa namna gani utapata manufaa kwa kuisaidia jamii, na mengine mengi

TAFADHARI UNAOMBWA KUCHANGIA ILI KUENDELEZA UFANISI WA BLOGU HII KWA MAANA MCHANGO WAKO UNASAIDIA SANA KATIKA KUHAKIKISHA ZOEZI LA UTAFITI ILI KUTOA ELIMU KWA KINA NA KWA UKAMILIFU. TAFADHARI UNAOMBWA KUCHANGIA KUPITIA NAMBA YA M-PESA 0752393944.
CHANGIA ILI KUKUZA UFANISI WA BLOG HII MCHANGO WAKO NDO NGUZO NA MSINGI WA KUPEANA UFANISI CHANGIA SASA.

NB: NAKALA HII BADO IPO KWENYE MABORESHO

Asante sana kwa kusoma nakala hii.

Awadhi Chang'a.
Geographer & Environmentalist.
awadhchang@outlook.com
0752-393944.

Thursday, April 2, 2015

HEKIMA HUSAIDIA KUTOA MAAMUZI SAHIHI

Hekima ni hali bora ya mtu katika kutambua ukweli wa binadamu, vitu, matukio na mazingira mbalimbali hata kuchagua vizuri la kufanya.
Katika dini mbalimbali inatokana na imani kwa Mungu.
Katika Ukristo inatajwa pengine kati ya vipaji vya roho mtakatifu vinavyokamilisha maadili ya kiutu na maadili ya kimungu vilevile (http://sw.wikipedia.org/wiki/Hekima).

Kwa ujumla, hekima ni uadilifu mzuri alionao mtu.

Katika kufanya maamuzi katika maisha yetu, hekima ndo ngao madhubuti ya kukuepusha kufanya maamuzi yasiyo sahihi kwa sababu binadamu walio wengi hufanya maamuzi yasiyo sahihi ambayo baadaye huleta madhara kwao na kwa jamii husika inayowazunguka kwa sababu ya kukosa hekima nafsini mwao.

Unapotaka kufanya maamuzi yoyote tumia hekima, kwa sababu hekima hujikita katika kutoa ukweli na uhalisia wa mambo, vilevile hekima hujitenga mbali na uongo vitu ambavyo ni vikwazo vikuu vya kufanya maamuzi kwa maana unapokua na hekima mala zoote utaegemea kwenye ukweli na uhalisia wa mambo yanayokuzunguka.

Kiongozi yoyote anahitaji hekima kwani wao ndo wanahusika katika kufanya maamuzi ya mwisho ya kundi ambalo analiongoza, kwa hiyo mtu yoyote anayekosa hekima hafai kuwa kiongozi kwa maana atakuwa anafanya maamuzi yasiyo sahihi ambayo hupotosha kundi ambalo analiongoza.

TUNAHITAJI KUFANYA MAAMUZI SAHIHI KWA AJILI YA MAENDELEO, KILA MMOJA WETU ANAHITAJI KUFANYA MAAMUZI SAHIHI.
ANZA SASA FANYA MAAMUZI SAHIHI.

Asante sana kwa kusoma nakala hii.
Awadhi Changa.
Geographer & Environmentalist.
awadhchang@outlook.com
0752-393944.

Wednesday, September 10, 2014

KAULI ILIYOSAHIHI INATOKA WAPI?, JIFUNZE KUONGEA MAMBO SAHIHI


FIRST DRAFT.
Maamuzi yoyote kabla ya kufikiwa ni lazima kuna kauli mbalimbali zinatolewa ili kufikia lengo mahususi,     
Kutoa kauli ni jambo kubwa sana ambalo linahitaji umakini mkubwa sana, kwani maneno yako yanaweza kuleta mabadiliko kwako na kwa mtu ambaye unamueleza, Kwa hiyo kutoa kauli sahihi au kuongea maneno sahihi kwa wakati sahihi husaidia sana kuleta mabadiliko. kwa hiyo unatakiwa kuwa makini sana unapo ongea mambo mbalimbali.
Unapo ongea kuna vitu lazima utambue kuna mambo yakuzingatia, moja ya mambo hayo ni kuzingatia kama mada hiyo ni ya wazi au si ya wazi (public or not). 

Faida ya kuongea mambo ambayo ni sahihi husaidia mtu kuwa huru na kulinda utu na heshima na kukuza status yako.

Inatakiwa kuvi expose vitu ulivyonavyo ili watu wajue vitu ulivyonavyo japokua ni lazima ujue kutenga vitu ambavyo ni hidden na vitu vya wazi. 

Pia unapotoa taarifa yoyote jitahidi kutoa taarifa ambayo ni sahihi na kuepuka kauli ambazo si sahihi kwa sababu UKWELI DAIMA HUMUWEKA MTU HURU.

Epuka kutoa taarifa ambazo hazijathibitishwa, Watu wengi hupenda kutoa taarifa ambazo wamesikia kwa watu wengine jambo ambalo si sahihi. Kimsingi unaweza ukathibitisha kauli ambazo si sahihi na kujikuta unapotosha na kujenga taswira mbaya.

Asante Sana.
Awadhi Chang'a.
Geographer -Environmentalist.

Tuesday, September 9, 2014

USIRUHUSU MTU AJUE UDHAIFU WAKO.

FIRST DRAFT. 

Maendeleo ni mabadiliko chanya, Maisha ni safari ndefu ambayo inahitaji uvumilivu sana hasa kwa maisha ya kitanzania au Afrika kwa ujumla, vijana wengi wa Tanzania wamekua wakihitaji mafanikio kwa haraka zaidi jambo ambalo kimsingi si sahihi kwa sababu huwezi kufika juu kabla ya kuanza chini ambako lazima ujenge msingi imara utakaokuwezesha kusimama imara, kwa sababu mala nyingi usipojenga msingi mzuri kwa maana ya ( mwanzo au maandalizi) mazuri huwezi kuwa na maisha bora yaliyo endelevu, maisha bora endelevu ni maisha mazuri yasiyo na kikomo.

Kujenga msingi imara ni sifa kubwa ya kujenga maisha mazuri yasiyo na kikomo, watu wengi hufanya mambo pasipokua kujua namna ya kuyafanya kwa sababu wamekosa uelewa wa namna ya kuyafanya mambo hayo. 

Elimu ni muhimu sana kujenga msingi mzuri wa maisha endelevu japo watu wengi wanajua ELIMU NI LAZIMA UKAE DARASANI UFUNDISHWE NA MWALIMU, jambo ambalo kimsingi si sahihi, elimu yoyote uitakayo utaipata ukijituma kusikiliza au kusoma maandiko mbalimbali ya vitabu, majarida, kupitia mtandao / internet. 

Usisikilize maneno ambayo hayajengi (Maneno yenye mtazamo hasi) kutoka kwa watu , mara nyingi watu huwa na maneno yenye mtazamo hasi ambayo kimsingi hurudisha nyuma kama utayatafakari kwa undani zaidi, Kaa na ushinde na watu wenye mitazamo chanya ambayo inauelekeo wa maendeleo. Daima utajifunza mbinu nzuri ambazo zitakusaidia kujenga msingi wa maisha endelevu. 

Panga mipango yako kwa ufasaha na umakini mzuri.

Weka kumbukumbu za mipango yako ya baadaye, Mpango wowote ambao utakujia akilini mwako ni vizuri ukauandikia maandishi na kuyatunza kwa sababu unaweza ukasahau kama unamambo mengi ya kuyashughulikia. Kuweka kumbukumbu husaidia kutumia fursa zozote zitakazojitokeza mbeleyako, kwa maana unaweza ukapata fursa hapo baadaye ukashindwa kuzitumia fursa hizo kwa kuwa na mawazo na Fikra finyu. 
 

Usiruhusu mtu ajue udhaifu wako, kwani kama ni adui yako anaweza kutumia udhaifu wako kukushusha ki-fikra, kwa sababu kushindwa kwa mtu huanzia kwanza katika fikra ndipo kujidhihirisha katika mazingira halisi kwa sababu binadamu hufanya maamuzi kutokana na mambo yaliyomo katika fikra zake. IF YOU THINK SMALL YOU WILL BE SMALL IN YOUR LIFE AND VISE VERSA.

MIPANGO MIZURI YA MAENDELEO HUJA PALE UNAPOKUA KATIKA CHANGAMOTO ZA KIMAENDELEO, KWA HIYO NI VIZURI KUKUMBUKA KUANDIKIA MIPANGO HIYO KABLA HUJAKUTANA NA FURSA.  

mfano mzuri ni huyu jamaa hapa chini anahitaji msaada;
NAHITAJI USHAURI WENU GUYS. BE SERIOUS.
Juzi nilikua napitia Ukurasa wa Vodacom Tanzania nikakuta wameweka Tangazo lao la M-PESA lenye hiyo picha wakihamasisha watanzania wajiunge na Taasisi ya Utoaji mikopo iitwayo TANZANIA LOANS ambayo Vodacom wameingia nao mkataba. Hii Taasisi inatoa mikopo bila RIBA.
Nilisoma tangazo lao na kupuuzia nikawa najua ni matapeli hao wametengeneza page feki ya Vodacom nikaipotezea, sasa jana asubuhi nikakuta tena Tangazo katika ukurasa wa ukweli wa msanii Lady Jaydee nae kapewa dili la kufanya matangazo kuhusu mikopo ya TANZANIA LOANS pia sikua na uhakika nayo.
Usiku wa jana huo huo nikaona sasa Tangazo rasmi katika TV ilikua TBC1 walirusha Live hilo Tangazo katika Taarifa ya Habari za kibiashara wakatoa mpaka website ya Online mtu anaweza kujiunga na akapatiwa mkopo wa pesa na atarudisha mkopo wa pesa bila kua na RIBA halafu marejesho yao mazuri hawambani mkopaji.
Nikasema ngoja nijaribu kujiunga nione je? Niukweli wanatoa mikopo?? Nikafungua website yao jana usiku http tanzania-Loans.wapka.mobi nikasoma maelezo yote! Kuna fomu nikaikuta nikaijaza, nilipoijaza fomu nikapokea ujumbe kua nimefanikiwa kujiunga natakiwa kulipia ada ya Uanachama Tshs. 95,000 (ELFU TISINI NA TANO) ili maombi yangu ya mkopo yaweze kuidhinishwa nipatiwe mkopo. Nikawa naogopa kulipia nisije kutapeliwa bure!
Sasa leo Asubuhi kuna jamaa yangu kumbe nayeye ameshawahi kujiunga na wakampatia kweli mkopo nikamuelezea akanitoa hofu! Nikaona kwani elfu95 na kitu gani?? Ngoja nijaribu nikawatumia elfu95 katika M-PESA wakanitumia ujumbe kua wameipokea pesa nisubirie ndani ya dakika30Nikasubiria, kweli wakanitumia mkopo kupitia M-PESA asubuhi hii ya leo muda si mrefu, niliomba mkopo wa Tshs. 3,000,000 (Million 3) hapo nilipo siamini friends.
‪#‎USHAURI‬: Nifungue mradi gani nina hizi Million Tatu, kwani nilikua sijajipanga nilifanya kama najaribu tu sikua na imani kama ntapata kweli huu mkopo nimejaribu wamenipa! Sijajua biashara ipi ambayo inalipa sana?? Please nisaidieni Mawazo yenu nawaomba! Utani tuweke kando nipo serious katika suala hili nahitaji ushauri wenu. Pia kwa yoyote ambae atahitaji kutembelea tovuti ya hawa jamaa wa mikopo, bonyeza hapa: http://tanzania-Loans.wapka.mobiNAHITAJI USHAURI WENU GUYS. BE SERIOUS.
Juzi nilikua napitia Ukurasa wa Vodacom Tanzania nikakuta wameweka Tangazo lao la M-PESA lenye hiyo picha wakihamasisha watanzania wajiunge na Taasisi ya Utoaji mikopo iitwayo TANZANIA LOANS ambayo Vodacom wameingia nao mkataba. Hii Taasisi inatoa mikopo bila RIBA.
Nilisoma tangazo lao na kupuuzia nikawa najua ni matapeli hao wametengeneza page feki ya Vodacom nikaipotezea, sasa jana asubuhi nikakuta tena Tangazo katika ukurasa wa ukweli wa msanii Lady Jaydee nae kapewa dili la kufanya matangazo kuhusu mikopo ya TANZANIA LOANS pia sikua na uhakika nayo.
Usiku wa jana huo huo nikaona sasa Tangazo rasmi katika TV ilikua TBC1 walirusha Live hilo Tangazo katika Taarifa ya Habari za kibiashara wakatoa mpaka website ya Online mtu anaweza kujiunga na akapatiwa mkopo wa pesa na atarudisha mkopo wa pesa bila kua na RIBA halafu marejesho yao mazuri hawambani mkopaji.
Nikasema ngoja nijaribu kujiunga nione je? Niukweli wanatoa mikopo?? Nikafungua website yao jana usiku http tanzania-Loans.wapka.mobi nikasoma maelezo yote! Kuna fomu nikaikuta nikaijaza, nilipoijaza fomu nikapokea ujumbe kua nimefanikiwa kujiunga natakiwa kulipia ada ya Uanachama Tshs. 95,000 (ELFU TISINI NA TANO) ili maombi yangu ya mkopo yaweze kuidhinishwa nipatiwe mkopo. Nikawa naogopa kulipia nisije kutapeliwa bure!
Sasa leo Asubuhi kuna jamaa yangu kumbe nayeye ameshawahi kujiunga na wakampatia kweli mkopo nikamuelezea akanitoa hofu! Nikaona kwani elfu95 na kitu gani?? Ngoja nijaribu nikawatumia elfu95 katika M-PESA wakanitumia ujumbe kua wameipokea pesa nisubirie ndani ya dakika30Nikasubiria, kweli wakanitumia mkopo kupitia M-PESA asubuhi hii ya leo muda si mrefu, niliomba mkopo wa Tshs. 3,000,000 (Million 3) hapo nilipo siamini friends.
#USHAURI: Nifungue mradi gani nina hizi Million Tatu, kwani nilikua sijajipanga nilifanya kama najaribu tu sikua na imani kama ntapata kweli huu mkopo nimejaribu wamenipa! Sijajua biashara ipi ambayo inalipa sana?? Please nisaidieni Mawazo yenu nawaomba! Utani tuweke kando nipo serious katika suala hili nahitaji ushauri wenu. Pia kwa yoyote ambae atahitaji kutembelea tovuti ya hawa jamaa wa mikopo, bonyeza hapa: http://tanzania-Loans.wapka.mobi

MIPANGO MIZURI YA MAENDELEO HUJA PALE UNAPOKUA KATIKA CHANGAMOTO ZA KIMAENDELEO, KWA HIYO NI VIZURI KUKUMBUKA KUANDIKIA MIPANGO HIYO KABLA HUJAKUTANA NA FURSA.
  
Asante sana.
Awadhi Chang'a.
Geographer & Environmentalist.






Friday, August 29, 2014

MTAZAMO CHANYA HUMJENGA MTU KI-FIKRA.

Kuna baadhi ya binadamu ambao huathiriwa kwa kiasi kikubwa na mawazo na maneno yenye mitazamo hasi ambayo huyapata kutoka kwa wengine, Hii pia ni kawaida tu hasa kwa binadamu yoyote ambaye ambaye ameshapitia misukosuko mbalimbali katika maisha yake ya kila siku. Watu wa namna hii wanahitaji sana mitizamo chanya ambayo Itawajenga ki-fikra,
Kwa sababu wakikumbuka walikotoka na maneno hasi uliyowapa kwaida hujikuta wakiwa wanyonge na walio kata tamaa, Tafadhari fikiri chanya, Ongea mitazamo chanya itakusaidia wewe pamoja na yule unayemueleza. kwa sababu unapoongea mitizamo chanya mala kwa mala, mitizamo hiyo chanya hujiweka katika ufahamu wako na kujikuta unafanya mambo mazuri ya maendeleo.
Ni vizuri sana kufanya, kuongea na kufikiri mitazamo chanya japokua mtazamo chanya hauwezi kujidhihirisha pasipokuwepo na mtizamo hasi kwa maana ili mtizamo chanya ujidhihilishe ni lazima kuwepo na mtizamo hasi kwa hiyo tufanye mitizamo chanya bila kusahau  kuwepo kwa mitazamo hasi ambayo pia ni vizuri kuitambua kusudi kuiepuka na kuikataa ili isikurudishe nyuma kwa maana ya kwamba tuitizame mitazamo hasi pia kwa kuitafutia sululisho la ukweli na uhakika kwa sababu "mtizamo chanya huwezi kuwepo pasipo mtizamo hasi kuwepo". Kwani majukumu ni kuyakabili kwanza.
Na mwisho kabisa kuna mtazamo ambao humuweka mtu katikati "neutral" ambao ni mtazamo ambao mda mwingi haufungamani na upande wowote ule, ambao mala nyingi husaidia kujiepusha na mazara ya kuegamia au kupendelea upande mmoja ambao mala nyingi hutumiwa na viongozi katika kutatua mijadala na mizozo ya makundi mbalimbali ambapo ni VIONGOZI huutumia ili kuleta suruhu. Vilevile ni vizuri kuwatoa watu wenye mitizamo Hasi na kuwapeleka kwenye kundi la watu wenye mitizamo chanya ambao unawajenga, Mbinu Hii  hutumiwa KUSULULISHA MIGOGORO NA MIZOZO MIKUBWA, mfano mzuri wa kiongozi makini ambaye hutumia mbinu hii nzuri ya kutatua Migogoro ni MH. JAKAYA MRISHO KIKWETE ambaye ni Raisi pekee wa Tanzania ambaye anaweza kutatua mizozo ya kisiasa yenye mivutano ya pande mbili, mfano katika hotuba yake ya ufunguzi wa BUNGE LA KUUNDA KATIBA MPYA alijitahidi kuwa kwenye mitizamo ya makundi yote na kutoa faida na hasara za Mitizamo ya makundi hayo na mwisho kabisa akajitahidi kuwavuta wale wenye mitizamo hasi ili wawe kwenye kundi la mtazamo chanya ili wawe wamoja au kitu kimoja na Hii ndo SIFA PEKEE YA MH RAISI J.K aliyonayo ambayo pia ilimfanya awe raisi bora wa Afrika na kupata tuzo ya utawala bora Afrika kwa sababu alishawahi kuwaweka pamoja makundi mawili yaliyokua  yanavutana KENYA ambapo tofauti zao zilisababisha kutokea kwa machafuko nchini mwao. KWA KWELI RAISI J.K ANASTAHILI PONGEZI MAALUM KWANI NI RAISI PEKEE WA TANZANIA ANAYEKUZA DEMOKRASIA, UELEWA (Elimu) NA UHURU, UKWELI KWA WANANCHI.
Mtizamo huu ni mzuri lakini ni vizuri kujitahidi kuegemea kwenye mtizamo chanya kwa sababu hauna madhara malanyingi HUMJENGA MTU NA KUMUEPUSHA NA MISUKOSUKO.
Mtazamo Chanya humjenga mtu kwa sababu mambo unayoyafikiri siku zote ndo zao kuu la maisha yako ya baadae kwa hiyo kama Unamtazamo chanya kwa kufikiria na kufanya mambo yako baasi jihesabie ya kwamba ni mtu mwenye maisha mazuri siku za usoni au za hapo baadaye, vile vile mambo yote unayoyafikilia huwa ndo muelekeo wako wa baadaye "IF YOU THINK SMALL YOU WILL BE SMALL ON YOUR LIFE".  
Hebu angalia mfano huu mdogo wa A Lincolin ambaye kimtazamo alitaka kurudishwa nyuma lakini hakukubaliana na hari kama hiyo kwa hiyo USIKUBALI KURUDISHWA NYUMA KWA MANENO MATUPU TU, Kwani wengine hujiona WAMESHINDWA kwa sababu ya maneno hasi ya watu, na kujikuta Wanafikiria kushindwa, ambapo fikra hizo hujengeka nafsini / akilini mwao na kujikuta wameshindwa kwa sababu fikra hizo zimejengeka akilini na nafsini mwao. SI VIBAYA KAMA UTAKUA UNAFIKIRI MITIZAMO CHANYA KWA SABABU ITAKUJENGA. Lakini si vibaya sana kama utajifunza kuitetea mitazamo yako CHANYA popote pale na kwa mtu yoyote. kwa maana mitizamo chanya huanza kujidhihirisha kutoka kwenye fikra hadi kwenye utekelezaji na utendaji wako.



"ALWAYS THINK POSITIVE TO RECEIVE POSITIVITY"
"UNAPOTEMBEA ANGALIA MBELE USITEMBEE UKIANGALIA NYUMA UTAANGUKA" 
Thanks
Awadhi Chang'a
Geographer & Enviromentalist


Thursday, August 28, 2014

JIFUNZE KUTUMIA FURSA ULIZO NAZO sehemu ya 1.

UBUNIFU ni sifa kubwa sana za kukuwezesha mradi wako uendelee vizuri na kupata mafanikio kwa maana ili uweze kufanikisha mradi wako ni lazima uwe na jambo jipya ambalo watu watalipokea kwa muamko mkubwa kwa maana mambo mapya hupendwa zaid au huwa na soko kubwa sana.
Wajasiliamali/Wafanyabiashara wanashauliwa kuwa wabunifu kwa maana watapata masoko kwa bidhaa zao kwa sababu utakua peke yako kwa hiyo utapata wateja wengi sana tofauti na kufanya biashara ambazo kila mtu anazifanya katika eneo lako kwa hiyo itapunguza ushindani katika biashara na kukupa fursa wewe za kufanikiwa, kwa mfano ukifungua duka la nafaka sehemu ambayo kuna maduka ya nafaka ni kokosekana kwa UBUNIFU katika kazi zako kwa hiyo hutaendelea mbele zaid.
Ubunifu unaweza kuupata wapi? au mambo yanayoweza kukusaidia kuwa mbunifu?, Kujifunza nchi za Nje au jirani wanafanya nini kwa wakati huu Mfano KUTEMBELEA NCHI ZA JIRANI, Ukweli wa mambo ni kwamba mambo mengi hutoka nchi za jirani na kuja kwetu Tanzania, kwa hiyo kilichofika Tanzania BASI NCHI ZA WENZETU KIMECHAKAA, Ni mambo machache ambayo huanzia hapa kwetu, asilimia kubwa yanatoka nje kwa hiyo jifunze ni nini wanafanya nchi za wenzetu afu unaweza ukapata ujuzi na kukuza maalifa juu ya kitu hicho na kukifanyia kazi.
VILE VILE kuboresha UBUNIFU wa mwenzio pia ni mbinu mojawapo ya kukuwezesha kutoka na kitu kipya ambacho kitakubaliwa na wakazi wote.
Kufanya TAFITI itasaidia sana kutoka na kitu kipya ambacho kitaleta manufaa kwako  na mwisho kabisa ni KUJIELIMISHA kwa kusoma majarida, magazeti, kutumia mtandao/ internet, taarifa mbalimbali.
Kwa mfano mzuri kabisa, Fursa zilizopo sasa zinatoka kwenye Umoja wa Afrika Mashariki ambao kwa sasa wanalengo la kukuza mahusiano ya kiuchumi, kisiasa na kijamiii ambao wana muelekeo wa kuja kuwa kama taifa moja lililo ungana kiuchumi, kisiasa na kijammii. kwa hiyo watanzania wanatakiwa kutafuta UBUNIFU kutoka kwa majirani zetu ili kujiendeleza kiuchumi, milango ipo wazi sasa na kazi ni kwako KUTUMIA FURSA.

Asante;
Awadhi Chang'a
Geographer.


Wednesday, August 27, 2014

NENO NI SILAHA.

TUJIFUNZE KUFANYA TAFITI, KUSOMA NA KUELEWA MAMBO NDIPO TUTOE KAULI NA KUONGEA MAMBO... USISIKIE TU JAMBO NA KUKURUPUKA KULITOA NA KULISAMBAZA KWANI MANENO NI SILAHA AMBAYO INAWEZA KUALIBU AU KUTENGENEZA JAMBO VILE VILE NENO LINAWEZA KUMUALIBU MTU AU KUMPA AHUENI MTU... KWA HIYO USITHUBUTU KUONGEA JAMBO BILA KUFANYA UTAFITI, UKISHINDWA WAACHE WENGINE WALIFANYIE HITIMISHO NA KULITOLEA MAAMUZI.
Awadhi Chang'a - Geographer